21-03-2022

Ufungulifu rasmi wa mwezi wa missioni katika CBCA

Imefanyika leo tarehe 20 March 2022 kwenye kanisa la 3e CBCA Virunga/Goma katika ibada ya shukrani kwa ajili ya kazi ya injili ya wachungaji 15 ambao walitangulia hapo mbeleni.

Ibada hii ikielekea ukingo wake, muchungaji Prezidenti na Kiongozi mkuu wa shirika, Rd. Dr Samuel Ngayihembako, aliweza kueleza maana yakuwepo kwa mwezi huu, ukiwa ni kutokana na azimio ya 42ème AG kuhusu umisheni. Azimio hii inasema hivi, kuona kwamba shamba imepanuka sana na hii ni baraka kwa kanisa, kuona kwamba juma la mission interne halikupata mapato mengi kwa mwaka 2021, na haikufikia mangojeo yetu, ikatupeleka kusaidia sehemu mbili tu, Lubumbaji na Bunia, kuona mahitaji ya shamba mupya ni mengi, mkutano uliamua:

« Azimio N°02/42ème AG/CBCA/2021 »

-Juma la mission interne litayarishwe kwa mwezi muzima na wachungaji wabadilishwe kama tulivyofanya wakati wa juma la mission externe…..
-DEVE kwa ushirikiano na Poste, wagawe vijiji vya
shamba mupya kwa makanisa makubwa makubwa za shirika. Makanisa haya ya parrainer vijiji hivyo na kuweza kuvikomalisha….
-Juma la pasaka litakaswe kuwa juma la mission interne.
-Kila kanisa iwe na kamati ya marafiki wa mission ambao watafuatilia kazi za mission ; na kufanya mobilisation katika usharika wao. Marafiki wa mission wawe wengi, ili wakiwa mufano 100000 na kila moja anaahidi kutoa 1$, mufuko wa mission utakuwa na 100000$ kwa mwaka. Hii itasaidia sana mahitaji ya shamba mupya.
-DEVE kwa ushirikiano na kamati za marafiki wa mission wawe wakipanga kila mwakashamba itakayohudumiwa mbele ya Assemblée Générale, ili watu wajitoe wakijua ile tunayotarajia kufanya mwakani. Hii itasidia kamati za marafiki wa mission kwa mobilisation.

Ni kwa maelezo haya ndiyo Prezidenti na Kiongozi mkuu wa shirika, aliweza kualika wakristo wote kuufanya mwezi wa misheni kua mwezi wao, wakijihakikishia kwamba kila mmoja kwa uwezo wake ame sapoti kazi ya misheni katika shirika.

« Kufatana na hayo, natangaza ufungulifu rasmi wa mwezi wa mission katika shirika letu la CBCA, katika jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, Amina », alinena hivo Rd. Dr Samuel Ngayihembako.

0 commentaire(s)

Aucun commentaire pour l'instant...

Laissez un commentaire